Monday, November 4, 2013

RUHUSA YA KUSOMA MASOMO 2 YA KUFUNDISHIA KWA WANAFUNZI WA B.ED

Tunapenda kuwajulisha wanafunzi wanaosoma B.ED waliojiunga na chuo kwa mwaka wa masomo 2011/2012 na 2012/2013 kuwa nao wanaruhusiwa kusoma masomo mawili ya kufundishia (teaching subjects) kwa kufuata muongozo wa wanafunzi wapya wa B.Ed wa mwaka huu mpya wa masomo 2013/2014 kama inavyojionesha katika Prospectors ya mwaka huu 2013/2014.
Kwa atakayependa kusoma masomo hayo 2 ya kufundishia, atahitajika kusoma units 12 kwa somo kuu (major) na units 6 kwa somo la pili (minor).
ZINGATIA:
Suala hili ni la hiyari kwa wanafunzi wa 2011/2012 na 2012/2013, lakini ni la lazima kwa wanafunzi wapya wa B.Ed wa mwaka huu wa masomo 2013/2014.
Tunawatia ufanisi mwema katika masomo yenu.

No comments:

Post a Comment