Monday, April 22, 2013

ZAYA MUDA WA KUJISAJILI KWA MITIHANI

Tunapenda kuwajulisha wanafunzi wote wa OUT kuwa tarehe ya mwisho ya kujisajili kwa mitihani ya June 2013 imesogezwa mbele mpaka tarehe 5 May 2013. Kutokana na kuwa tarehe hiyo itaangukia siku ya Jumapili, tunawashauri mkamilishe malipo husika kabla ya Ijumaa ya tarehe 3 May 2013 (ambayo ni siku ya kazi) ili  tuweze kuingiza taarifa za malipo yenu kwenye akaunti zenu za SARIS, na hivyo kuweza kuruhusiwa kujisajili. Tafadhali zingaia.

Tuesday, April 16, 2013

USAJILI WA WANAFUNZI WALIOZIDISHA MIAKA 8 YA MASOMO

Chuo kikuu huria cha Tanzania kinawatangazia wanafunzi wote waliozidisha miaka 8 ya masomo (wenye namba za usajili ...../T.04 kurudi nyuma) kuwa chuo kinadhamiria kuwafutia usajili wao wa masomo kutokana na kuzidisha muda unaokubalika kisheria.
Hivyo, yeyote anayehusika anahitajika kumuandikia barua DVC (Academic)  akieleza sababu zilizomfanya azidishe muda na kuomba kuongezewa muda wa kukamilisha masomo. Barua hizo zipitie kwa Mkurugenzi wa kituo (DRC), na ziambatanishwe na nakala ya SARIS ya mwanafunzi husika pamoja na ushahidi wa sababu atakazozieleza. Mwisho wa kuandika barua hizo ni tarehe 19 June 2013. Kwa kushindwa kufanya hivyo, mwanafunzi husika atakuwa amejifuta chuo mwenyewe. OUT Tanga Centre inawatkia utekelezaji mwema wa agizo hilo.

Monday, April 15, 2013

MWISHO WA USAJILI WA MITIHANI YA JUNE 2013

Wanafunzi wote mnakumbushwa kuwa tarehe ya mwisho ya usajili wa masomo, ulipaji ada na usajili wa mitihani ya June 2013 imekaribia. Hivyo, kamilisha malipo yako ya ada na usajili wa kozi pamoja na mitihani mapema ili kuepuka msongamano katika siku ya mwisho. Mwisho  ni Jumamosi ya tarehe 20/04/2013.  OUT Tanga Centre inakutakia uwajibikaji mwema.

Monday, April 8, 2013

TAREHE YA MWISHO YA FACE-TO-FACE

Wanafunzi wote wa OUT Tanga mnakumbushwa kuwa siku ya mwisho ya kufanya Portfolio Assessment ni Alhamisi, tarehe 11 April 2013. Hivyo, hakikisha kuwa unapata assessment kabla ya muda huo kuisha. Itakuwa ni vigumu kufanya assessment yoyote baada ya tarehe hiyo kutokana na walimu kukabiliwa na majukumu mengine.
Zingatia.

Wednesday, April 3, 2013

COMMENCEMENT OF FACE-TO-FACE WEEK!

To all OUT students (Tanga),
We once again remind you that face-to-face week is going to begin next Saturday, on 6th April 2013. So, each of you (students) is required to attend the first day as there will be some important information to be announced. We wish you good journey to the centre, and happy belated Easter.